
Na Mwandishi Wetu
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) upande wa Tanzania Bara anatarajiwa kuchaguliwa katika Mkutano Mkuu wa chama hicho tawala utakaofanyika Januari 18 na 19, 2025 jijini Dodoma.
Nafasi hiyo ilikuwa wazi tangu Julai 2024 kutokana na kujiuzulu kwa aliyekuwa akiishikilia, Abdulrhaman Omar Kinana.
Kwa mujibu wa Katibu wa Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Amos Makalla, wajumbe wa mkutano huo watazungumzia ajenda tatu ambazo ni kumchagua Makamu Mwenyekiti CCM wa Tanzania Bara na kupokea taarifa za utkelekezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020-2025.
Mada nyingine ni kupokea taarifa za utendaji wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinmduzi ya Zanzibar.
Mkutano Mkuu wa CCM ndicho kikao cha juu zaidi cha chama hicho kikongwe barani Afrika, ambacho hutoa maamuzi ya uongozi wa nchi.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>Mwenyekiti mpya MISA Tanzania awatembelea wadau wa habari Kanda ya Ziwa
>>Rais Samia ateua viongozi mbalimbali, Mhandisi Lwamo sasa Katibu Mtendaji Tume ya Madini Tanzania
>>Siasa: Mbowe awashangaa wanaomtaka ang’atuke uenyekiti CHADEMA
>>Tume ya Madini yatoa tahadhari ongezeko la matumizi ya baruti nchini
No comments:
Post a Comment